• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Kibarua akana kuiba Vaseline

Kibarua akana kuiba Vaseline

Na RICHARD MUNGUTI

KIBARUA aliye na umri wa miaka 24 ameshtakiwa kumnyang’anya mwanamke mafuta ya Vaseline Jelly na Sabuni ya Rexona.

Isiah Munabi alikana alimnyang’anya kimabavu Vivian Awuor.Hakimu mkuu mahakama ya Milimani Susan Shitubi alifahamishwa Munabi alimkabili Awuor mwendo wa saa nne usiku katika eneo la Upper Hill Nairobi na kumshambulia.

Munabi alimtisha mlalamishi kisha akamrukia kumnyang’anya mkoba wake uliokuwa na mafuta ya Vaseline, Veroline, Rozari, kalamu mbili na Sabuni ya Rexona zote za thamani ya Sh1000. Polisi waliokuwa wanashika doria katika eneo hilo la Link Road, Upper Hill walimpata mshtakiwa akimenyana na mlalamishi.

Polisi walimfukuza na kumkamata mshtakiwa na kurejesha mkoba wa mlalamishi. Mshtakiwa alikana shtaka na kuachiliwa kwa dhamana ya pesa tasilimu Sh80,000. Kesi hiyo imeorodheshwa kusikizwa Machi 3,2022.

You can share this post!

Matumizi ya trei kukuza miche ya mahindi hasa maeneo kame

Raia wa Pakistan asababisha kioja kortini

T L