Na MASHIRIKA
HARARE, ZIMBABWE
RAIS wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amemkabidhi makamu wake mamlaka ya kuendesha nchi kwa siku 23 huku akienda likizoni.
Mnangagwa alianza likizo yake Ijumaa na atarejelea mamlaka yake Februari 5, 2022.
Naibu wa Rais Constantine Chiwenga ambaye pia ni Waziri wa Afya, ataendesha nchi kwa muda huo ambao Rais Mnangagwa atakuwa likizoni.
“Wakati huo ambao Rais atakuwa likizoni makamu wa rais Chiwenga atakuwa kaimu rais,” ikasema taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Rais na Baraza la Mawaziri Misheck Sibanda.