• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 12:11 PM
Biden aahidi kuweka wazi endapo atatetea urais

Biden aahidi kuweka wazi endapo atatetea urais

 NA MASHIRIKA

WASHINGTON, AMERIKA

RAIS wa Amerika, Joe Biden alisema mnamo Jumatano kuwa atatangaza mapema mwaka ujao – 2023 – iwapo atagombea tena urais.

Alikuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari katika Ikulu ya White House jijini Washington DC katika hafla ambayo Wademocrat walikuwa wakielezea kuridhika kwao na matokeo ya uchaguzi wa katikati ya muhula.

Biden, mwenye umri wa miaka 79, na ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwarai wapigakura kuwachagua wanasiasa wa chama cha Demokratic, alielezea furaha yake baada ya matokeo kuashiria kwamba huenda chama cha Republican kisipate viti vingi kwenye mabaraza yote mawili ya bunge, kama ilivyotabiriwa na wachambuzi.

Rais Biden aliongeza kwamba chama chake kimefanya vizuri akiongeza kwamba ndio mwanzo wa mazuri kutoka kwa chama chake cha Democrats.

“Tumefanya vizuri. Huu ni mwanzo tu,” Biden alisema.

Waandishi wawili wa habari walitaka kujua kama atagombea muhula wa pili, na kama atafanya hivyo, ni lini atatangaza azma yake.

“Nafikiri kila mtu anataka nigombee urais, lakini tutajadiliana kuhusu suala hilo. Sioni haja ya kuharakisha uamuzi huo, kwa njia moja au nyingine, iwe ni kesho, kesho kutwa au wakati mwingine wowote. Nadhani itakuwa mapema mwaka ujao ambapo nitafanya uamuzi huo,” Rais Biden akasema.

Udhibiti wa Baraza la Seneti la Marekani haukuwa umebainika wazi mnamo Jumatano usiku huku Warepublican wakikaribia kupata wabunge wengi wa baraza la wawakilishi.

Hayo yalijiri siku moja baada ya Wademocrat kuvuka matarajio ya wengi katika uchaguzi wa katikati ya muhula wa Marekani.

Matokeo ya mashindano ya kuwania viti vya Seneti katika majimbo ya Nevada na Arizona, ambako viongozi walioko madarakani wa chama cha Democrats walikuwa wakimenyana na wapinzani wa Republican, bado hayajatangazwa rasmi, huku maelfu ya kura zikiwa bado hazijahesabiwa.

Iwapo vyama hivyo vitagawanya viti hivyo, basi hatima ya Seneti itaangukia katika uchaguzi wa marudio wa Georgia kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka miwili.

Hayo yatafanyika baada ya Edison Research kukadiria kuwa si mwaniaji aliyemaliza muda wake wa chama cha Demokratic.

Wengine ni Raphael Warnock na Herschel Walker wa Republican ambaye angefikia asilimia 50 ya kura zinazohitajika ili kuepusha uchaguzi wa marudio mnamo Desemba 6, 2022.
  • Tags

You can share this post!

Dalali aachiliwa kwa dhamana ya Sh200,000

KASHESHE: Amwaga povu zito

T L