NA SINDA MATIKO
ALIKIBA anasema sababu moja inayofanya muziki wa Afrika Mashariki kukwama na kushindwa kwenda mbali ni ubinafsi.
Kulingana na King Kiba, wa kulaumia ni wasanii wa Kenya na Tanzania sababu wamejawa ubinafsi.
“Kwa ujumla nitazungumzia jambo lililo wazi. Ili kuuza na kutangaza muziki, unahitaji umati. Ndio sababu Wanigeria na Waafrika Kusini wanatoboa sababu wanaonea fahari muziki wao. Wanapigana sapoti sana wenyewe kwa wenyewe. Wana koneksheni za nguvu na wana umoja kutuliko sisi. Itatuchukua muda kufika levo zao,” Kiba kamwaga.