• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 6:26 PM
Popcaan aahirisha shoo yake Nairobi kwa mara nyingine, hadi Aprili 16, 2022

Popcaan aahirisha shoo yake Nairobi kwa mara nyingine, hadi Aprili 16, 2022

Na CHARLES WASONGA

MASHABIKI wa mwanamuziki, Andre Hugh Sutherland, maarufu kama Popcaan, wamevunjika moyo baada yake kuahirisha shoo yake nchini.

Kwenye ujumbe katika akaunti yake ya twitter Popcaan alisema shoo yake ambayo ilisubiriwa kwa hamu sasa imehamishwa hadi Aprili 16, 2022. Awali, shoo hiyo ilikuwa imeratibiwa kufanyika mnamo Januari 8 kabla ya kusukumwa hadi Februari 26, 2022 na sasa imeahirishwa tena hadi Aprili 16 mwaka huu jijini Nairobi.

“Niaje Nairobi, sasa ni rasmi kwamba baada ya maombi mengi kutoka kwa mashabiki wangu kutoka Kenya, Vibesonly Kenya imesukuma mbela shoo hiyo jijini Nairobi hadi Aprili 16, 2022. Tushirikiane ili kuifanya shoo hiyo iwe ya kihistoria,” Popcaan akaeleza.

Kuahirishwa kwa shoo hiyo kunajiri baada ya Popcaan kufanya shoo kubwa nchini Gambia. Hata hivyo mwanamuziki huyo alipatwa na mkosi baada ya simu yake chapa iPhone kuibiwa na watu wasiojulikana. Popcaan alianza kupata umaarufu katika rubaa ya kimataifa baada ya kuchomoa wimbo wake kwa jina, Clarks.

Endapo atatua Kenya mnamo Aprili, 16, 2022 alivyopanga, mwanamuziki huyo ataongezwa kwenye orodha ya wanamuziki wa asili ya Jamaica kuwahi kufika nchini. Miongoni mwao ni, Koshens. Etana na Charly Black.

You can share this post!

Himizo wakulima wazalishe mazao salama kuwahi soko la...

Jinsi ya uzuia maambukizi ya kila mara ya UTI

T L