Na CITIZEN
DAR ES SALAAM, TANZANIA
RAIS Samia Suluhu wa Tanzania amewatema mawaziri waliokuwa washirika wa karibu wa marehemu John Magufuli, kwenye hatua inayoonekana kuwa juhudi za kuimarisha udhibiti wake katika baraza hilo.
Kwenye mageuzi hayo, mawaziri waliotemwa ni William Lukuvi, Kitila Mkumbo, Prof Palamagamba Kabudi na Geoffrey Mwambe (Uwekezaji).
Wadadisi wanasema lengo la Rais Suluhu ni kupunguza upinzani ambao amekuwa akikumbwa nao kutoka kwa baadhi ya mawaziri, ikizingatiwa baadhi yao wanalenga kuwania nyadhifa mbalimbali za kisiasa kwenye uchaguzi mkuu wa 2025.
Hatua hiyo inajiri siku moja baada ya Spika wa Bunge la Kitaifa Job Ndugai kujiuzulu, kwa kutoa matamshi yaliyofasiriwa “kuiingilia” serikali.