• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:02 PM
Samia atema washirika wa Magufuli

Samia atema washirika wa Magufuli

Na CITIZEN

DAR ES SALAAM, TANZANIA

RAIS Samia Suluhu wa Tanzania amewatema mawaziri waliokuwa washirika wa karibu wa marehemu John Magufuli, kwenye hatua inayoonekana kuwa juhudi za kuimarisha udhibiti wake katika baraza hilo.

Kwenye mageuzi hayo, mawaziri waliotemwa ni William Lukuvi, Kitila Mkumbo, Prof Palamagamba Kabudi na Geoffrey Mwambe (Uwekezaji).

Wadadisi wanasema lengo la Rais Suluhu ni kupunguza upinzani ambao amekuwa akikumbwa nao kutoka kwa baadhi ya mawaziri, ikizingatiwa baadhi yao wanalenga kuwania nyadhifa mbalimbali za kisiasa kwenye uchaguzi mkuu wa 2025.

Hatua hiyo inajiri siku moja baada ya Spika wa Bunge la Kitaifa Job Ndugai kujiuzulu, kwa kutoa matamshi yaliyofasiriwa “kuiingilia” serikali.

You can share this post!

Vihiga Bullets yazoa ushindi wa kwanza kwa kutandika Wazito...

TALANTA YANGU: Dogo mkali wa mitindo

T L