• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:50 AM
Zari: Siwezi kurudiana na Diamond ila ni mshikaji wangu sana

Zari: Siwezi kurudiana na Diamond ila ni mshikaji wangu sana

NA RAJAB ZAWADI

KAMA kuna ma-ex ambao wameendelea kuwavuruga mashabiki wao kuhusiana na ukaribu wao, basi ni soshiolaiti Zari Hassan na supastaa Diamond Platnumz.

Wawili hawa waliwahi kutesa sana walipokuwa wapenzi kwa takriban miaka minne, uhusiano ulioishia wao kujaliwa watoto wawili.

Lakini toka waachane miaka imepita zaidi sita sasa, wawili hao wameendelea kuonyesha kuwa na mahusiano mazuri kupita maelezo.

Ukaribu wao umewapelekea baadhi ya mashabiki wao kuhisi ni kana kwamba huenda siku moja wawili hao wakarudiana endapo mahusiano yao ya sasa yataingia mdudu.

Kwa sasa Diamond yupo na msanii wake Zuchu kama mpenzi wake huku Zari akiwa kwenye ndoa na kijana mdogo Shakib Lutaaya.

Hata hivyo, Zari anasema hata ikitokea kwamba wajikute wote wapo singo–yani yeye na Diamond–kamwe hawawezi kurudiana licha ya wengi kuhisi ni kana kwamba bado wanapendana kutokana na baadhi ya matukio yao ya ulavidavi.

Lakini Zari anasisitiza kuwa huo ni ushikaji tu na wala hamna la ziada.

“Diamond atasalia kuwa baba kwa wanangu na hilo halina mjadala. Ni rafiki yangu kwa sababu sisi sio wale ma-ex wanaochukiana, ma-ex wenye machungu. Sisi huongea, ni mtu ambaye ninaweza kumpigia simu kama kuna kitu kinasumbua na yeye vile vile. Kwa hiyo hamna damu mbaya baina yetu. Kwa hiyo mnaponiona na yeye hakuna kitu chochote eti ooh wamerudiana. Hapana… hakuwezi kuwa na kitu kama hicho. Sisi ni marafiki na wazazi tu basi,” Zari kanyoosha.

Wawili hao wamejaliwa mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane Princess Tiffah na kijanadume mwenye umri wa miaka saba Prince Nillan.

Imekusanywa na SINDA MATIKO

  • Tags

You can share this post!

Kuppet yalia kucheleweshwa kwa pesa za walimu...

Muuzaji bangi ang’ata na kurarua mdomo wa polisi...

T L