• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
FAUSTINE NGILA: DCI ijitahidi kung’amua mbinu za wizi mitandaoni

FAUSTINE NGILA: DCI ijitahidi kung’amua mbinu za wizi mitandaoni

Na FAUSTINE NGILA

HAPO Jumatatu, Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) ilichapisha kwenye Facebook kisa cha kustaajabisha kuhusu jinsi ‘mfu’ aliiba mamilioni ya ‘mfu’ mwenzake.

Katika maelezo yake, DCI ilisema kuwa wahuni wa mitandaoni walitumia simu ya mtu aliyefariki kuiba Sh2.8 milioni katika akaunti ya benki ya Mkenya mwingine aliyeaga dunia.

Kivipi? Walitumia simu ya mmoja wa wafu hao, ambayo ilikuwa imepotea, kupora pesa katika akaunti zake kwanza kabla ya kuitumia kuiba hela katika akaunti ya pili.

Wakenya wengi walidai kisa kama hicho kinatokana na ukosefu wa ajira kwa vijana walio na digrii, lakini sikubaliani nao kwani katika mtandao huo wa majambazi watano, niliona watu waliopitisha umri wa miaka 50.

Kuwa na ujuzi wa kiteknolojia kamwe haukupi uhuru wa kuutumia kunyanyasa Wakenya wenzako na hilo ni kosa linalopaswa kuadhibiwa vikali.Swali kuu ni kuhusu jinsi walifanikiwa kutoa kadiwia au kadi ya simu yenye nambari iliyosajiliwa na Safaricom, Airtel au Telkom na kupata nenosiri inayotumika katika sajili zote za benki.

DCI wanafaa kuchunguza ni vipi wakora hao waliweza kupata kuingia kwenye programu za simu za benki za NCBA, Co-operative, Equity na vipi walifaulu kuzituma hela hizo kwa akaunti nyingine na kuzitoa.

Mara nyingi nimezungumzia uwezo wa teknolojia ya ‘blockchain’ katika kuzima wizi huu, lakini Kenya inaonekana haijajitayarisha kuwekeza kwa teknolojia hii. Iwapo mtu amefariki, hela zake benki zinapaswa kutolewa tu na familia yake pekee, ambayo inafaa kujua nenosiri.

Awali nimeipongeza Safaricom kwa kujaribu kuleta ubunifu wa kutumia uso wa mwenye kadi ya simu kama neno siri, lakini kwa simu za bei ya chini zisizowezesha teknolojia hiyo, wezi hutoa kadi na kuibadilisha kwa kufuta nenosiri ya kwanza.Lakini ndipo ubadilishe nywila hii, lazima utambue nywila ya awali.

Na ndipo uibe mamilioni, lazima ung’amue nenosiri ya akaunti ya benki ya pili ambapo unatuma hela hizo ili ukazitoe.Je, wahuni hawa ni wafanyakazi wa zamani wa benki hizi au kampuni hizi za mawasiliano?

Walijuaje watu hao wana hela nyingi kwa akaunti, na kuwa wamefariki? Safaricom, kwa mfano, mwaka uliopita ilitoboa tundu katika mtandao wa M-Pesa ilipoambia watumizi kuwa wanaweza kuteua mtu wa familia na kumpa nenosiri ili wakati wanapofariki, mtu huyo anaweza kutoa zile hela kwa manufaa ya familia.

Iwapo DCI, itachukua muda wake kupeleleza kwa makini, itapata kuwa kuna mtandao wa watu wa familia, wafanyakazi wa benki na wa kampuni za mawasiliano ambao wamekuwa wakishirikiana kuiba mamilioni ya pesa zinazoachwa na Wakenya waliokufa.

Naipongeza DCI kwa kazi kuntu inayofanya, na pia kampuni za benki na mawasilino kwa kukubali kushirikiana na wapelelezi kutoa taarifa zinazosaidia kukamatwa kwa wakora wa mitandaoni.L

akini kuelewa kwa kina jinsi ujambazi huu unaendeshwa kutasaidia kuzima ndoto za mamia ya vijana ambao wanategemea kupora matunda ya jasho la watu wanapokufa.

[email protected]

You can share this post!

MAUYA OMAUYA: Nyachae alikuwa na bidii, ila alikuwa...

Raila ataka kesi za kupinga BBI zitupiliwe mbali