• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:39 PM
Jinsi ya kuandaa buns zenye ufuta  

Jinsi ya kuandaa buns zenye ufuta  

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 30

Muda wa mapishi au uokaji rasmi: Dakika 45

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • unga wa ngano gramu 500
  • sukari vijiko 2 vikubwa
  • chumvi
  • maji kikombe kimoja na nusu
  • mafuta ya kupikia vijiko 2 vikubwa
  • hamira kijiko kikubwa
  • yai moja
  • mbegu za ufuta

Maelekezo

Weka unga kwenye bakuli, tia sukari, chumvi, hamira, mafuta na yai. Kisha mimina maji kidogo kidogo na uanze kukanda unga wako.

Hakikisha hauwi laini sana wala mgumu sana.

Baada ya kukanda, uache kwenye bakuli uumuke.

Ukisha umuka, katakata uwe kwa maumbo unayotaka.

Koroga ute wa yai. Paka ute huo kwenye kila donge.

Nyunyuzia mbegu za ufuta kwenye madonge yako.

Buns zenye ufuta . Picha/ Margaret Maina

Sasa yaweke kwenye chombo cha kuokea kisha acha tena yaumuke.

Dhibiti joto la ovena yako liwe ni nyuzi 250°C.

Kisha anza kuoka huku nyuzijoto zikiwa ni 180°C kwa dakika 45.

Epua na ufurahie kwa kuzila buns zikiwa zimeshapoa.

You can share this post!

Clarke Oduor asuka pasi kusaidia Barnsley kuokota alama...

TAHARIRI: Serikali isuluhishe uhaba wa walimu