Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 30
Muda wa mapishi au uokaji rasmi: Dakika 45
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Weka unga kwenye bakuli, tia sukari, chumvi, hamira, mafuta na yai. Kisha mimina maji kidogo kidogo na uanze kukanda unga wako.
Hakikisha hauwi laini sana wala mgumu sana.
Baada ya kukanda, uache kwenye bakuli uumuke.
Ukisha umuka, katakata uwe kwa maumbo unayotaka.
Koroga ute wa yai. Paka ute huo kwenye kila donge.
Nyunyuzia mbegu za ufuta kwenye madonge yako.
Sasa yaweke kwenye chombo cha kuokea kisha acha tena yaumuke.
Dhibiti joto la ovena yako liwe ni nyuzi 250°C.
Kisha anza kuoka huku nyuzijoto zikiwa ni 180°C kwa dakika 45.
Epua na ufurahie kwa kuzila buns zikiwa zimeshapoa.