• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
KASHESHE: Bado pasua kichwa!

KASHESHE: Bado pasua kichwa!

NA SINDA MATIKO

NDOA ya AliKiba na mkewe Mkenya Amina Khaleef bado haipo sawa.

Toka taarifa za Amina kuwasilisha kesi mahakamani akiomba talaka kumekuwa na ukimya.

Baadhi ya blogu zimedai kuwa Ali na mkewe wameshatengeneza mambo na kwamba wapo sawa. Hata hivyo kulingana na mdokezi aliyepiga stori na safu hii, ndoa hiyo bado ipo hoi.

“Wale ni watu wangu wa karibu sana na Amina mwenyewe nafikiri anataka kuendelea na mchakato wa talaka. Kiba anatamani wayamalize ili ndoa yao irudi lakini Amina kidogo anasita. Anasisitiza kuwa lazima amfunze jamaa adabu kwa kumvunjia heshima kwa sababu yeye alikuwa ameamua kutulia ila jamaa akaamua kuwa mjanja,” katupia mdokezi.

Taarifa za talaka aidha zimemharibia dili kadhaa Kiba kwa mujibu wa mdokezi huyo, na anahofia kuwa inaweza ikamharibia hata zaidi endapo itarasimishwa.

You can share this post!

KIKOLEZO: Wueeh, kimemuumania!

KASHESHE: Kauli ya Ben Pol

T L