NA SINDA MATIKO
MSUPA Xenia Manasseh amekuwa staa wa hivi punde Mkenya, kuingizwa kwenye mradi wa EQUAL unaondeshwa na kampuni ya kusambaza na kupakia muziki Spotify.
Mradi huu, ulibuniwa mahususi kuwapiga sapoti wanamuziki wa kike ibukia.
“Hii ni heshima kubwa, wameniheshimisha na sikuichukulia kawaida sana. Sapoti kama hizi ndizo zinatuweka mjini baadhi yetu,” amesema Manasseh.
Mastaa wengine Wakenya waliofanikiwa kuingia kwenye mradi wa EQUAL ni pamoja na Nikita Kering, Muthoni The Drummer Queen na Silvia Ssaru.