• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
KIKOLEZO: Walirejea baada ya kustaafu!

KIKOLEZO: Walirejea baada ya kustaafu!

NA SINDA MATIKO

JUZI Cristiano Ronaldo katangaza anauza ndege yake ya kibinafsi kwa sababu imekuwa ndogo kutokana na familia yake kupanuka. Sasa anataka kununua kubwa kidogo.

Ndio maisha waishiyo mastaa wengi. Huwezi ukawalaumu. Wengine baada ya kupiga pesa waliamua kustaafu kabisa. Hivi ukiwa na pesa zinazotosha kununua Kisiwa chako binafsi na yoti, na pipa, utasita kustaafu?

Kuna ambao walishaamua sanaa imetosha, wakajitoa ila kwa sababu moja au nyingine, iwe fedha au mapenzi ya sanaa, wakaamua kuoga na kurudi soko. Hawa Kwa mfano.

CAMEROON DIAZ

Astaafu: 2014

Arejea: 2022

Cameron Diaz. PICHA | HISANI

Miaka minane baada ya kustaafu uigizaji, staa Diaz kaamua kurudi kwenye gemu mwaka huu. Filamu yake ya mwisho ilikuwa Annie aliyoigiza na Jamie Foxx ila sasa anarudi na mzigo mwingine Back In Action, utakaomshirikisha Foxx tena. Filamu hiyo itaanza kutengenezwa mwishoni mwa mwaka huu.

JULIA ROBERTS

Astaafu: 2002

Arejea: 2022

Julia Roberts. PICHA | HISANI

Huwezi kuamini Julia Roberts kaamua kurudi kwenye gemu baada ya miaka 20. Julia alistaafu hata kabla YouTube haijaingia Kenya. Umeme kule kwetu kijijini ulikuwa wazo lisilofikirika. Leo kijiji chawaka mwanga. Julia alistaafu hata kabla ya kuwepo kwa 4G. Lakini sasa ameamua kurudi ili kuwachekesha watu kwenye filamu ya Ticket to Paradise pamoja na George Clooney.

CRAIG DANIEL

Mwigizaji raia wa Uingereza Daniel Craig wakati wa kuonyeshwa kwa filamu ya James Bond ‘Spectre’ jijini Paris, Ufaransa, Oktoba 29, 2015. PICHA | AFP

Astaafu: 2015

Arejea: 2019

Baada ya filamu ya James Bond Spectre kutoka 2015, Craig aliulizwa kama ataigiza tena kama James Bond na kusema hana mipango hiyo. Alistaafu kabla ya kurejea tena mwaka uliofuata.

Baada ya filamu ya No Time To Die, 2019, akatangaza kustaafu tena. Kwa sasa anasema anataka kujikita zaidi na utayarishaji wa filamu shughuli atakayoipiga nyuma ya pazia.

JAY Z

Astaafu: 2003

Arejea: 2006

Jay-Z ahudhuria makala ya 18 ya 40/40 Club jijini New York mnamo Agosti 28, 2021. PICHA | AFP

Hata kabla hajawa bilionea aliye kwa sasa, Jay Z akiwa na umri wa miaka 33, alitangaza kustaafu muziki mara tu baada ya kudondosha albamu ya The Black Anthem. Kipindi hicho alidai kuboeka na kuendelea kufanya muziki. Lakini 2006, alirejea na albamu mpya Kingdom Come na mpaka leo hii anafanya muziki kwa kujisikia.

EMMA WATSON

Astaafu: 2006

Arejea: 2010

Staa huyu wa Harry Potter alitangaza kustaafu 2007 akiwa na umri wa miaka 17 tu. Kufikia 2007 alikuwa tayari amehusika kwenye filamu tano kubwa zilizofanya vizuri.

“Nina pesa za kutosha za kula hadi nife,” alijigamba kipindi hicho. Filamu ya mwisho ya Harry Potter ilitoka 2010. Alikaa kimya kidogo kabla ya kurejea kwa kishindo akishiriki kwenye filamu kadhaa kubwa kama The Circle and The Beauty and The Beast.

ALEC BALDWIN

Mwigizaji Alec Baldwin akihudhuria shoo ya “The Public” mjini Toronto, Ontario, Canada, Septemba 09, 2018. PICHA | AFP

Astaafu: 2014

Sababu zake za kustaafu 2014 ni mapaparazzi waliokuwa wakimfuatilia sana kutokana na kuwa nyota yake ilikuwa iking’aa sana. Hakufurahia hicho na akaamua kustaafu. Lakini haikumchukua muda kabla yake kuhusika kwenye filamu zingine kubwa kama Mission: Impossible na Rogue Nation.

  • Tags

You can share this post!

KIPWANI: Eti katulia ila umkutapo studio, ni balaa!

DOMO: Msikizeni shangazi, ana neno!

T L