• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 12:52 PM
LISHE: Jinsi ya kuandaa chips masala

LISHE: Jinsi ya kuandaa chips masala

Na MARGARET MAINA

[email protected]

HIKI ni chakula maarufu kinachopendwa na wengi kwa sababu ni rahisi kukiandaa.

Muda wa kuandaa: Dakika 30

Muda wa mapishi: Dakika 30

Walaji: 5

Vinavyohitajika

  • viazi kilo mbili vilivyokatwa kama chips
  • nyanya 4 zilizosagwa kwa blenda
  • kitunguu maji 1 kilichokatwakatwa
  • pilipili mboga 1 iliyokatwakatwa
  • dania
  • kitunguu saumu kijiko 1
  • pilipili manga kijiko 1
  • currypowder kijiko 1 kidogo
  • nyanya ya mkebe vijiko 2
  • pilipili ya unga (masala) ingawa sio lazima
  • mafuta ya kupikia

Maelekezo

Mimina mafuta kwenye kikaangio na yakishika moto weka chips uzikange. Hakikisha zinakuwa kavu kwa sababu chips kavu ndizo nzuri kwa mapishi ya chips masala. Zikishaiva, zitoe kwenye mafuta uziweke pembeni uendelee na matayarisho mengine.

Weka sufuria ulotia mafuta mekoni na yakishika moto weka kitunguu maji ukikaange mpaka kiwe rangi ya kahawia.

Weka pilipili manga, currypowder na kitunguu saumu na upike kwa dakika mbili.

Weka pilipili mboga na dania upike kwa sekunde kadhaa.

Sasa weka nyanya iliyosagwa, nyanya ya mkebe na chumvi kisha funika kwa dakika tano mpaka ziive.

Weka chips uchanganye vizuri. Hakikisha unachanganya kwa makini ili chips zisibondeke.

Epua, pakua na ufurahie.

You can share this post!

Hospitali mpya zimehudumia wagonjwa 16,000 jijini –...

Jinsi ya kuandaa smoothie ya ndizi na parachichi