NA MWORIA MUCHINA
KASUKU kwa jina Kea, wanapatikana kwa wingi nchini New Zealand.
Kasuku hawa wa rangi ya kijani zamani walipenda kula matunda na mbegu lakini wakati wakazi wa maeneo wanakopatikana kwa wingi walianza kufuga kondoo, ndege hao walibadilisha lishe na kuanza kuwavamia kondoo hao kwa midomo yao mikali na kula mafuta kwenye miili ya kondoo hao.
Kasuku hao hutoa sauti inayofanana na ile ya paka, na wamekuwa tishio kubwa kwa ufugaji wa kondoo nchini humo.