Na MARGARET MAINA
Walaji : 3
Kuandaa kuku unahitaji
Vinavyohitajika ili kuandaa katlesi
Maelekezo
Weka mnofu wa kuku pamoja na vitu vingine katika sufuria ili uchemshe mekoni kama kawaida ili nyama iive vizuri.
Chemsha viazi kwa chumvi kiasi kisha chuja maji yote na uviponde.
Nyambue kuku kupata vipande vidogovidogo. Unaweza ukasaga pia kwa blenda ya vitu vikavu ukitaka kazi yako iwe rahisi.
Mimina mafuta ya kupikia kwenye sufuria mekoni na yakishapata moto, tia vitunguu na kaanga hadi vianze kupata rangi ya kahawia.
Tia tangawizi na saumu pamoja na maji kidogo kisha kaanga kwa dakika tatu.
Tia manjano na chumvi kiasi halafu koroga vizuri kisha tia kuku na kaanga tena kwa dakika mbili. Baada ya hapo, tia viazi vyako ulivyoponda na uchanganye vizuri.
Tia viungo vilivyobaki kisha koroga vizuri. Onja ujue kama chumvi ni ya kutosha au unatakikana kuiongeza.
Epua na acha mchanganyiko upoe.
Chota mchanganyiko wako na ufanye maduara kisha taratibu binya kwa kiganja chako na ufinye. Panga katika sahani. (Unaweza fanya shepu yoyote)
Mimina mafuta katika sufuria iliyo mekoni na mafuta yakipata moto, chovya katlesi katika mayai kisha zungusha katika chenga za mkate na tia katika mafuta moto.
Kaanga hadi zipate rangi ya kahawia pande zote mbili.
Epua katika chujio zichuje mafuta. Pakua na ufurahie.