• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Tosti ya stroberi

Tosti ya stroberi

NA MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 30

Muda wa mapishi: Dakika 15

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • mkate slesi 16
  • kikombe ½ cha lozi iliyokatwa (si lazima)
  • kikombe 1 cha stroberi zilizogandishwa, zimeyeyushwa, na kutengenezwa zikawa juisi
  • kikombe ½ cha sukari nyeupe
  • vijiko 2 vya unga wa mahindi
  • kikombe ½ cha jibini laini ya krimu
  • kijiko 1 cha vanilla
  • kikombe 1 cha maziwa
  • mayai 3 yaliyopigwa
  • kijiko ½ cha mdalasini
  • kijiko ¼ cha kungumanga ya kusaga
  • vijiko 2 vya siagi

Maelekezo

Pika na ukoroge lozi kwenye sufuria kwenye moto wa wastani hadi iwe na harufu nzuri. Kaanga kwa muda wa dakika tano.

Koroga sukari nusu kikombe na wanga pamoja kwenye sufuria juu ya moto wa wastani.

Ongezea stroberi kwenye mchanganyiko wa sukari huku ukiendelea kukoroga kwa takriban dakika tano.

Changanya jibini ya krimu, vijiko viwili vya sukari, na vanilla pamoja kwenye bakuli.

Changanya maziwa, mayai, vijiko viwili vya sukari, mdalasini, na kungumanga pamoja katika bakuli.

Paka mchanganyiko wa stroberi, jibini ya krimu, vijiko viwili vya sukari, na vanilla kwenye slesi zako.

Chovya vipande vya mkate kwenye mchanganyiko wa yai.

Yeyusha siagi kwenye sufuria kwenye moto wa wastani.

Pika slesi zako hadi ziwe na rangi ya kahawia – kwa dakika tatu kila upande.

  • Tags

You can share this post!

Utawala wa Uhuru wang’aa katika ujenzi wa barabara

Tumia mchele kutengeneza sabuni yenye manufaa tele kwa...

T L