Na MARGARET MAINA
UNAWEZA ukatumia maganda ya machungwa kwa urembo.
Kukabili tatizo la vinyweleo usoni
Maganda ya machungwa huondoa vinyweleo usoni.
Wanawake wengi hulalamikia tatizo la kutokwa na vinyweleo vingi kwenye miili yao.
Kupambana na hali hii, baadhi yao hutumia wembe ambapo badala ya kuvipunguza, husababisha viongezeke na ngozi za nyuso zao kuzeeka. Badala ya kutumia krimu kali au wembe, maganda ya machungwa yanaweza kukusaidia kuondoa vinyweleo hivyo.
Vinavyohitajika
* Unaweza kuandaa unga huo kwa kuyakausha maganda hayo juani kwa siku kadhaa kisha ukayatwanga na kuyasaga kupata ungaunga wake.
Namna ya kuandaa
Changanya unga wa maganda ya machungwa au malimau na unga wa mtama kwenye chombo kimoja kisha ongeza mafuta ya mzeituni pamoja na maji ya waridi. Changanya mpaka upate ujiuji mzito.
Jipake ujiuji huo usoni na uache ukae kwa dakika 10. Baada ya hapo, tumia vidole vyako vya mikono kuisugua ngozi yako kwa namna ya kutengeneza mduara. Fanya hivi kwa dakika 10 kisha baada ya hapo, osha uso wako kwa maji safi. Fanya hivyo kila siku kwa kipindi cha wiki mbili hadi tatu na bila shaka utaona mabadiliko.
Tumia maganda ya machungwa kutoa mba kichwani
Watu wengi wanasumbuliwa na ugonjwa wa mba kichwani. Mara nyingi mba hutokea nyakati za baridi kwani kichwa huwa ni kikavu sana kwa kipindi chote hicho. Kama unasumbuliwa na hilo tatizo, unatakiwa kuwa makini na mafuta unayotumia na kuhakikisha unatumia mafuta kila unapoosha nywele zako.
Jinsi ya kufanya
Chukua chungwa ulimenye upate maganda yake. Baada ya hapo, chukua limau likamue kisha uweke kwenye blenda usage hadi uwe na mchanganyiko mmoja.
Matumizi
Osha nywele zako kwanza zitakate na baada ya hapo, zikaushe kisha paka mchanganyiko wako kwenye ngozi. Acha kwa muda wa dakika 20 kisha osha kwa kutumia shampuu unayotumia ambayo unaamini ni nzuri.
Tumia tiba hii kwa wiki mara tatu na utaona jinsi utakavyokomesha moja kwa moja tatizo la mba kichwani.