• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 3:46 PM
TUSIJE TUKASAHAU: Wito wa Rais Kenyatta kaunti zilipe madeni usigeuzwe wimbo

TUSIJE TUKASAHAU: Wito wa Rais Kenyatta kaunti zilipe madeni usigeuzwe wimbo

RIPOTI ya hivi punde iliyotolewa na Afisi ya Msimamizi wa Bajeti (CoB) Margaret Nyakang’o, inasema kuwa kaunti zote 47 zinadaiwa jumla ya Sh105 bilioni na wanakandarasi na wafanyabiashara, huku ikisalia miezi minne kabla ya uchaguzi wa Agosti 9.

Kulingana na ripoti hiyo, magavana 11 kati ya 21 ambao wanahudumu muhula wa pili na wa mwisho, ni miongoni mwa wale ambao wanadaiwa kiasi kikubwa cha fedha na wanakandarasi.

Kaunti za Narok, Mombasa, Embu, Murang’a na Embu ni miongoni mwa kaunti zinazozongwa na malimbikizo ya madeni ya karibu Sh2 bilioni, kila moja.

Lakini tusije tukasahau kuwa tangu Juni 2019, Rais Uhuru Kenyatta, amekuwa akizitaka asasi zote za serikali kuu na zile za kaunti, kulipa madeni yote yaliyothibitishwa kuwa halali.

Isitoshe, akisoma bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2021-2022 bungeni mnamo Juni 10, 2021, Waziri wa Fedha, Ukur Yatani, alitoa makataa ya hadi mwisho wa mwezi huo kwa magavana kulipa malimbikizi ya madeni.

Hata hivyo, kufikia sasa makataa hayo yameonekana kupuuzwa.

  • Tags

You can share this post!

Hofu Mlimani kuhusu unaibu rais

Safina yamtaka Jimi atafute urais kupitia tiketi yake

T L