• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 12:11 PM
AC Milan wakomoa Juventus katika Serie A na kuweka kocha Massimiliano Allegri katika hatari ya kupigwa kalamu

AC Milan wakomoa Juventus katika Serie A na kuweka kocha Massimiliano Allegri katika hatari ya kupigwa kalamu

Na MASHIRIKA

AC Milan waliendeleza masaibu ya kocha Massimiliano Allegri katika kikosi cha Juventus kwa kusajili ushindi wa 2-0 mnamo Jumamosi katika pambano la Ligi Kuu ya Italia (Serie A).

Milan wanaonolewa na kocha Stefano Pioli walijibwaga ugani kw ajili ya mechi hiyo wakiwa na kiu ya kujinyanyua baada ya Chelsea kuwapepepta 3-0 katika pambano la awali la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) jijini London, Uingereza.

Fikayo Tomori alifungulia Milan ukurasa wa mabao mwishoni mwa kipindi cha kwanza kabla ya Brahim Diaz kufanya mambo kuwa 2-0 mwanzoni mwa kipindi cha pili.

Matokeo hayo yalipaisha Milan hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa jedwali la Serie A kwa alama 20 sawa na Atalanta na Napoli wanaodhibiti kilele cha jedwali.

Hadi alipocheka na nyavu za Juventus, Tomori alikuwa amefunga bao moja pekee katika soka ya Italia tangu ajiunge na Milan kutoka Chelsea mnamo Januari 2021.

Milan walipoteza nafasi kadhaa za kufunga bao la tatu kupitia kwa fowadi wa zamani wa Liverpool, Divock Origi, aliyemwajibisha kipa Wojciech Szczesny.

Chini ya Allegri, Juventus hawajashinda mechi yoyote ya ugenini katika kampeni za mashindano mbalimbali msimu huu. Sasa wanashikilia nafasi ya nane jedwalini kwa alama 13.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

UJAUZITO NA UZAZI: Kukabili uvujaji damu baada ya kujifungua

Mbappe awapita Messi na Ronaldo orodha ya mastaa wakwasi...

T L