• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Arsenal kutamatisha mkataba wa Willian anayetaka kurejea Brazil

Arsenal kutamatisha mkataba wa Willian anayetaka kurejea Brazil

Na MASHIRIKA

ARSENAL wanapanga kuagana rasmi na kiungo wa zamani wa Chelsea, Willian Borges anayehusishwa uwezekano mkubwa wa kujiunga na klabu ya Corinthians nchini Brazil.

Kufaulu kwa mpango huo kutaokolea Arsenal mamilioni ya fedha ikizingatiwa kwamba Willian ambaye hulipwa Sh31 milioni kwa wiki, angali na miaka miwili kwenye mkataba wake wa miaka mitatu na Arsenal.

Willian, 33, alijiunga na Arsenal mwishoni mwa msimu wa 2019-20 baada ya kujiengua kambini mwa Chelsea. Japo aliwajibishwa katika mechi 25 za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), hajachezeshwa katika gozi lolote la muhula huu wa 2021-22.

Kabla ya kusakatwa kwa mechi iliyoshuhudia Arsenal wakipigwa 5-0 na mabingwa watetezi Manchester City katika EPL mnamo Agosti 28, 2021, kocha Mikel Arteta alikiri kwamba “haelewi sababu ya kipindi cha Willian ugani Emirates hakikuridhisha.”

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Umuhimu wa madini ya zinki mwilini

Everton kuachilia Moise Kean kurejea Juventus kujaza pengo...