Na MASHIRIKA
BEKI wa zamani wa Manchester United, Chris Smalling, alifungia AS Roma goli la pili katika ushindi wa 2-1 uliokuwa wao wa kwanza dhidi ya Inter Milan katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A) tangu Februari 2017.
Roma sasa wana alama 16, nne nyuma ya viongozi Napoli waliokomoa Torino 3-1. Mabingwa watetezi AC Milan wana pointi 17 baada ya kucharaza Empoli 3-1.
MATOKEO YA SERIE A (Jumamosi):
Inter Milan 1-2 AS Roma
Napoli 3-1 Torino
Empoli 1-3 AC Milan
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO