• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:55 AM
AS Roma yazamisha Leicester City na kutinga fainali ya Europa Conference League

AS Roma yazamisha Leicester City na kutinga fainali ya Europa Conference League

Na MASHIRIKA

LEICESTER City walikosa kufuzu kwa fainali ya kipute kipya cha Europa Conference League baada ya AS Roma kuwapokeza kichapo cha 1-0 katika mchuano wa mkondo wa pili wa nusu-fainali mnamo Alhamisi usiku katika uwanja wa Olimpico nchini Italia.

Bao la pekee na la ushindi kwa upande wa Roma lilijazwa kimiani na fowadi wa zamani wa Chelsea, Tammy Abraham katika dakika ya 11 na hivyo kuongoza waajiri wake kubandua Leicester kwa jumla ya magoli 2-1.

Leicester walishuka dimbani wakiwa na ulazima wa kushinda ili kufuzu kwa fainali ya soka ya bara Ulaya kwa mara ya kwanza katika historia baada ya kuambulia sare ya 1-1 katika mkondo wa kwanza wa nusu-fainali mnamo Aprili 28, 2021 ugani King Power.

Itakuwa mara ya kwanza tangu 1991 kwa Roma ya kocha Jose Mourinho kufuzu kwa fainali ya soka ya bara Ulaya itakayowakutanisha na Feyenoord ya Uholanzi iliyodengua Olimpique Marseille ya Ufaransa kwa jumla ya mabao 3-2 licha ya kuambulia sare tasa katika mkondo wa pili wa nusu-fainali.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Pigo kwa uchumi pato la kilimo likishuka mno

Wakufunzi Mikel Arteta na Jonas Eidevall watia saini...

T L