• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 10:50 AM
Barcelona kuvaana na Real Madrid kwenye fainali ya Spanish Super Cup baada ya kudengua Real Betis kwenye nusu-fainali

Barcelona kuvaana na Real Madrid kwenye fainali ya Spanish Super Cup baada ya kudengua Real Betis kwenye nusu-fainali

Na MASHIRIKA

BARCELONA watakutana sasa na watani wao wa tangu jadi, Real Madrid, kwenye fainali ya Spanish Super Cup msimu huu baada ya kudengua Real Betis kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 2-2 katika nusu-fainali mnamo Alhamisi usiku.

Robert Lewandowski aliwafungulia Barcelona ukurasa wa mabao katika dakika ya 40 kabla ya Ansu Fati kuwafungia goli la pili mwishoni mwa kipindi cha pili.

Hata hivyo, Nabil Fekir na Lorenzo Garcia walisawazishia Betis na kufanya mshindi wa mechi hiyo kuamuliwa kupitia penalti. Betis walikamilisha mechi wakiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Andres Guardado kuonyeshwa kadi nyekundu sekunde chache kabla ya kipenga cha kuashiria mwisho wa mchezo kupulizwa.

Real nao walifuzu kwa fainali baada ya kufunga Valencia penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ugani King Fahd jijini Riyadh, Saudi Arabia mnamo Jumatano usiku.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Man-United wamsajili fowadi Wout Weghorst wa Uholanzi kwa...

Fulham waendeleza masaibu ya kocha Graham Potter kambini...

T L