• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 8:50 AM
Kocha Xavi ashinda mechi yake ya kwanza akidhibiti mikoba ya Barcelona

Kocha Xavi ashinda mechi yake ya kwanza akidhibiti mikoba ya Barcelona

Na MASHIRIKA

MKUFUNZI Xavi Hernandez alianza kazi kambini mwa Barcelona kwa kuongoza kikosi hicho kusajili ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Espanyol uwanjani Camp Nou.

Barcelona waliponea chupuchupu katika mechi hiyo iliyoshuhudia wageni Espanyol wakipoteza nafasi nyingi za kufunga mabao katika kipindi cha pili.

Bao la pekee na la ushindi kwa upande wa Barcelona lilipachikwa wavuni na Memphis Depay kupitia penalti ya dakika ya 48.

Ushindi wa Barcelona uliwasaza katika nafasi ya sita kwa alama 20, nane nyuma ya Sevilla na Real Sociedad wanaoselelea kileleni mwa jedwali.

Xavi alichezea Barcelona mechi 767 na akawaongoza kutia kapuni mataji 25 katika kipindi cha miaka 17. Hadi aliporejea Uhispania kudhibiti mikoba ya Barcelona, Xavi alikuwa akinoa kikosi cha Al Sadd nchini Qatar.

Barcelona watavaana na Benfica ya Ureno ugani Camp Nou katika mchuano ujao wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA). Ushindi utawakatia tiketi ya kuingia hatua ya 16-bora ya kivumbi hicho.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kananu kaangukia minofu kweli

Liverpool wakomoa Arsenal na kupiga breki rekodi ya...

T L