• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 3:16 PM
Bayern wapepeta Hertha Berlin na kufungua pengo la alama 10 kileleni

Bayern wapepeta Hertha Berlin na kufungua pengo la alama 10 kileleni

Na MASHIRIKA

BAYERN Munich wataelekea nchini Qatar kwa fainali za Kombe la Dunia kwa Klabu (Fifa Club World Cup) wakijivunia kufungua mwanya wa alama 10 kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga).

Hii ni baada ya mabingwa hao watetezi wa Bundesliga wanaonolewa na kocha Hansi Flick kuwapepeta Hertha Berlin 1-0 kwenye mchuano wa Bundesliga mnamo Februari 5 na kufungua pengo la alama 10 kati yao na RB Leipzig kileleni mwa jedwali.

Bayern walitamalaki mchezo na kumiliki asilimia kubwa ya mpira katika mechi hiyo iliyoshuhudia fowadi Robert Lewandowski akipoteza penalti mwanzoni mwa kipindi cha kwanza.

Kingsley Coman ndiye aliyefunga bao la pekee na la ushindi katika mchuano huo baada ya kumwacha hoi kipa Rune Jarstein katika dakika ya 21.

Matokeo ya mechi hiyo yalisaza Hertha wakining’inia padogo mkiani mwa jedwali la Bundesliga kwa alama 17, tisa mbele ya Schalke wanaokokota nanga.

Bayern wameratibiwa kukutana na miamba wa soka ya Afrika Al Ahly ya Misri kwenye nusu-fainali ya Kombe la Dunia mnamo Jumatatu ya Februari 8, 2021.

Ni mchuano unawaweka Bayern katika nafasi nzuri ya kutia kapuni taji lao la sita chini ya kipindi cha miezi tisa iwapo wataibuka washindi wa Kombe la Dunia nchini Qatar.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Inter Milan wapiga Fiorentina na kutua kileleni mwa Serie A

Nina saini za wabunge 126 kumtimua Ruto – Savula