Na MASHIRIKA
INTER Milan walirejea kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Italia (Serie A) baada ya kuwapiga Fiorentina 2-0 mnamo Februari 5, 2021.
Kiungo Nicolo Barella aliwafungulia Inter ukurasa wa mabao katika dakika ya 31 kabla ya bao la fowadi wa zamani wa Manchester United, Romelu Lukaku kukataliwa na refa kwa madai kwamba alitikisa nyavu akiwa ameotea.
Ivan Perisic ndiye aliyefungia Inter ya kocha Antonio Conte bao la pili katika dakika ya 52 baada ya kushirikiana vilivyo na kiungo Achraf Hakimi.
Inter kwa sasa wnaajivunia alama 47, moja nyuma ya AC Milan ambao huenda wakarejea kileleni mwa jedwali mnamo Februari 7 iwapo watawalaza Crotone uwanjani San Siro.
TAFSIRI NA CHRIS ADUNGO