• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 6:50 AM
Benfica yakomoa Ajax na kuingia robo-fainali za UEFA

Benfica yakomoa Ajax na kuingia robo-fainali za UEFA

Na MASHIRIKA

DARWIN Nunez alifungia Benfica bao la pekee na la ushindi dhidi ya Ajax katika mchuano wa mkondo wa pili wa hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Jumanne usiku jijini Amsterdam, Uholanzi.

Ushindi huo uliwezesha Benfica ya Ureno kufuzu kwa robo-fainali za kipute hicho msimu huu kwa jumla ya mabao 3-2. Vikosi hivyo vilishuka dimbani kwa marudiano baada ya kuambulia sare ya 2-2 katika mkondo wa kwanza jijini Lisbon mnamo Februari 23, 2022.

Nunez aliwaweka Benfica uongozini mnamo Jumanne usiku katika dakika ya 77 baada ya kumwacha hoi kipa Andre Onana. Ajax walitamalaki mchezo na kumiliki asilimia kubwa ya mpira. Ingawa fowadi Sebastien Haller aliwafungia bao mwanzoni mwa kipindi cha kwanza, goli hilo halikuhesabiwa kwa kuwa Dusan Tadic alikuwa ameotea.

Licha ya Ajax kukita kambi langoni mwa wageni wao kwa muda mrefu, Benfica walisalia imara katika safu yao ya ulinzi chini ya Nicolas Otamendi beki wa zamani wa Ajax na Tottenham Hotspur, Jan Vertonghen.

Benfica kwa sasa wametinga robo-fainali za UEFA kwa mara ya kwanza tangu 2015-16.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Atletico Madrid yakatiza safari ya Man-United kwenye soka...

Makanisa, misikiti kuanza kupokea waumini wengi

T L