• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 9:55 AM
Brentford yazamisha chombo cha Southampton katika EPL

Brentford yazamisha chombo cha Southampton katika EPL

Na MASHIRIKA

MABAO mawili katika sekunde 79 za kipindi cha kwanza yaliwezesha Brentford kusajili ushindi muhimu wa 3-0 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Klabu hizo zilianza mechi kila moja ikijivunia alama 40. Hata hivyo, ushindi wa Brentford uliwapaisha hadi nafasi ya 12 ligini kwa alama 43 sawa na Newcastle na Aston Villa waliopepeta Burnley 3-1 ugani Turf Moor.

Brentford waliwekwa kifua mbele na Pontus Jansson katika dakika ya 13 sekunde chache kabla ya Yoane Wissa kufunga la pili. Kristoffer Ajer alifanya mambo kuwa 3-0 katika dakika ya 79.

Licha ya kushindwa, Southampton wangali na uhakika wa kusalia katika EPL msimu ujao ikizingatiwa kwamba wanakamata nafasi ya 15 kwa alama 40, nane zaidi kuliko Everton wanaokamata nafasi ya 18.

Southampton ambao wamesalia na mechi chache zaidi (mbili) miongoni mwa vikosi sita vya mwisho jedwalini, walikuwa katika nafasi ya tisa kwenye jedwali la EPL mnamo Februari.

Hata hivyo, wamepoteza mechi saba kati ya 10 zilizopita katika EPL huku wakisalia sasa na kibarua kizito zaidi dhidi ya Liverpool na Leicester City kwa usanjari huo.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

NYOTA WA WIKI: Ciro Immobile

11 kupambana mmoja wao awe mgombea mwenza wa Raila

T L