• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Cavani kujiunga na Boca Juniors ya Argentina baada ya mtakaba wake kukatika Man-United msimu huu

Cavani kujiunga na Boca Juniors ya Argentina baada ya mtakaba wake kukatika Man-United msimu huu

Na MASHIRIKA

FOWADI matata wa Manchester United na timu ya taifa ya Uruguay, Edinson Cavani, atajiunga na kikosi cha Boca Juniors mwishoni mwa msimu huu baada ya mkataba wake kutamatika rasmi ugani Old Trafford, Uingereza.

Cavani, 34, anatarajiwa kuwa huru kujiunga na kikosi chochote mwishoni mwa kampeni za msimu huu.

Japo Man-United walikuwa na fursa ya kurefusha kandarasi yake kwa mwaka mmoja zaidi, mshambuliaji huyo wa zamani wa Paris Saint-Germain (PSG) amehiari kurejea Amerika Kusini kuchezea Boca Juniors ya Argentina.

Kwa mujibu wa gazeti la Ole nchini Argentina ambalo limefichua kwamba Cavani atakuwa radhi kupunguziwa nusu ya mshahara wake wa sasa wa Sh29.4 milioni kwa wiki ili kutimiza ndoto ya kuchezea kikosi cha Boca Juniors alichoanza kukishabikia utotoni.

Cavani ambaye pia amewahi kuchezea kikosi cha Napoli nchini Italia, anatarajiwa kutia saini mkataba wa miaka mitatu kambini mwa Boca Juniors kwa matarajio kwamba atawaongoza kutwaa taji la Copa Libertadores kwa mara ya kwanza tangu 2007.

Kiini cha Boca Juniors kuwania maarifa ya Cavani ni haja ya kutaka mshambuliaji huyo awe kizibo cha nyota wa zamani wa Manchester City, Carlos Tevez ambaye mkataba wake na Boca unatamatika rasmi mwishoni mwa msimu huu wa 2020-21. Cavani ataungana na aliyekuwa beki wa Man-United, Marcos Rojo, kambini mwa Boca Juniors.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Ligi ya daraja la pili yapamba moto

Madhara yaletwayo na uvaaji wa viatu vyenye visigino virefu...