• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:50 AM
Chepng’etich na Kipruto mibabe Chicago Marathon

Chepng’etich na Kipruto mibabe Chicago Marathon

Tuzo

Nafasi tano za kwanza ziliandamana na tuzo ya Sh9.1 milioni, Sh6.6m, Sh5.4m, Sh3.6m na Sh3.0m mtawalia.

Chepng’etich alikosa pembemba Sh9.1m bonasi ya kuweka rekodi ya Chicago Marathon. Katika mbio zingine zilizofanyika Jumatatu, Bornes Kitur alitwaa umalkia wa Lisbon Marathon nchini Ureno kwa saa 2:24:17 akiwa ni Mkenya wa kwanza kufanya hivyo tangu Sarah Chepchirchir mwaka 2017.

Agnes Keino (2:23:26) na Philimon Kipchumba (2:07:28) walitawala Munich Marathon nchini Ujerumani wakiwa ni Wakenya wa kwanza kupata ufanisi huo tangu Michael Kite mwaka 2000.

Hildah Jepkosgei aliibuka mshindi katika Sofia Marathon kwa 2:45:52 nchini Bulgaria naye Naaman Serem akakamata nafasi ya pili (2:18:04). Pius Karanja (2:06:55) aliongoza Gevin Kerich (2:07:07) na Joshua Kemboi (2:08:09) kufagia nafasi tatu za kwanza Eindhoven Marathon nchini Uholanzi naye Paskalia Chepkosgei (2:22:47) akashinda kitengo cha kinadada.

  • Tags

You can share this post!

Green Eagle FC yabanduliwa nje Taifa Ngano Cup

Afisa ashauri wakazi kuwekeza kwa ufugaji samaki ili...

T L