NA ABDULRAHMAN SHERIFF
MABINGWA mara mbili wa Taifa Ngano Super Cup, Green Eagles FC ilibanduliwa nje ya mashindano ya Taifa Ngano Super Cup ilipofungwa mabao 2-1 na mahasimu wao Fetuwe FC kwenye mechi ya robo fainali.
Kwenye mchezo huo uliovutia halaiki ya mashabiki wa soka Mombasa na vitongoji vyake, Fetuwe ilijihakikishia ushindi kupitia kwa wafungaji Ali Ghalia na John Otieno.