• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 12:42 PM
Gor yapaa kileleni, AFC ikilemea Posta Rangers Ligi Kuu ya FKF

Gor yapaa kileleni, AFC ikilemea Posta Rangers Ligi Kuu ya FKF

Na WAANDISHI WETU

Gor Mahia jana ilipaa hadi kileleni mwa msimamo ya jedwali la Ligi Kuu huku AFC Leopards ikipata ushindi wao wa pili msimu huu.

K’Ogalo ilikuwa moto wa kuotea mbali huku ikiikalifisha wanyonge Vihiga Bullets 3-0 ugani Bukhungu. AFC Leopards ilifuta misururu ya matokeo mabaya ya kutoshinda katika mechi sita, ilipoipiga Posta Rangers 1-0 ugani Nyayo.

Katika mechi nyingine ya jana iliyotandazwa ugani Mbaraki Mombasa, wenyeji Bandari waliagana sare tasa dhidi ya KCB.Ugani Bukhungu, George ‘Black’ Odhiambo ambaye alirejea Gor msimu huu baada ya kutimuliwa na Tusker, jana alifungua ukurasa wa mabao baada ya kucheka na nyavu dakika 12.

Mvamizi wa Boniface Omondi alifunga bao jingine katika dakika ya 85 kabla ya Peter Lwasa kuzamisha kabisa chombo cha Vihiga Bullets kupitia shuti iliyojaa wavuni dakika ya 91.Ugani Nyayo ambao ulikuwa mwenyeji wa mechi za Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu Disemba 12 mwaka uliopita, Washington Munene alifunga kupitia mpira wa ikabu dakika ya 32.

Ingwe ilitawala mchezo huo na kabla ya ushindi huo, ilikuwa imeshinda Tusker 1-0 kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi mnamo Septemba 26. Jijini Mombasa KCB ilitawala kipindi kirefu cha dakika 45 za mwanzo ambapo washambulizi wake walipoteza nafasi kadhaa za kufunga huku Bandari ikifanya vizuri zaidi kipindi cha pili lakini hakuna iliyoweza kuona nyavu za mwenziwe.

Kufuatia ushindi wao, Gor sasa imepaa hadi kileleni mwa Ligi Kuu kwa alama 17 baada ya mechi saba, alama sawa na Kakamega Homeboyz ambayo ilitoka nyuma na kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya Mathare United mnamo Jumatano.

Ripoti za CECIL ODONGO, ABDULRAHMAN SHERIFF na JOHN ASHUHUNDU

You can share this post!

Dereva Varese kutifua vumbi Guru Nanak Rally

Mauaji: Polisi waashiria kukata rufaa

T L