• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Haaland afunga mabao mawili na kusaidia Dortmund kupepeta Besiktas kwenye UEFA

Haaland afunga mabao mawili na kusaidia Dortmund kupepeta Besiktas kwenye UEFA

Na MASHIRIKA

BORUSSIA Dortmund walikamilisha kampeni zao za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwa kutandika Besiktas 5-0 licha ya kufahamu kwamba hawakuwa na uwezo wa kufuzu kwa hatua ya makundi ya kivumbi hicho.

Donyell Malen aliwafungulia Dortmund ukurasa wa mabao baada ya kukamilisha krosi ya Jude Bellingham katika dakika ya 29 kabla ya kadi nyekundu ambayo Welinton wa Besiktas kutoa fursa kwa wenyeji kuteremkia wageni wao ugani Signal Iduna Park.

Welinton aliadhibiwa kwa kosa la kumchezea visivyo Mahmoud Dahoud ndani ya kijisanduku na Marco Reus akafunga kupitia penalti. Reus alifunga bao la pili katika dakika ya 53 kabla ya Erling Braut Haaland kupachika wavuni magoli mawili kunako dakika za 68 na 81.

Haaland, 21, alifunga bao lake la kwanza dakika tano pekee baada ya kutokea benchi. Nyota huyo raia wa Norway sasa amepachika wavuni mabao 23 kutokana na mechi 19 za UEFA. Dortmund walikuwa tayari na uhakika wa kukamilisha kampeni za makundi katika nafasi ya tatu huku Besiktas wakiambulia nafasi ya mwisho bila alama yoyote.

You can share this post!

Niko tayari kuwa mgombea mwenza wa Raila- Munya

KNEC yapuuzilia uvumi kwamba KCSE na KCPE imeahirishwa

T L