• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 9:50 AM
Harry Kane aongoza Spurs kucharaza Brighton katika mchuano wa EPL

Harry Kane aongoza Spurs kucharaza Brighton katika mchuano wa EPL

Na MASHIRIKA

HARRY Kane alifunga bao lake la nane msimu huu na kusaidia Tottenham Hotspur kupepeta Brighton 1-0 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Jumamosi.

Matokeo hayo yalisaza Spurs katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa jedwali la EPL kwa alama 20, tatu nyuma ya viongozi na mabingwa watetezi Manchester City.

Brighton kwa sasa wanakamata nafasi ya sita kwa pointi 14 sawa na Newcastle United. Nusura wafunge mabao kupitia kwa Lewis Dunk, Danny Welbeck na Solly March waliomtamtiza pakubwa kipa Hugo Lloris katika kipindi cha pili.

Spurs walishuka dimbani siku chache baada ya kocha wao wa viungo, Gian Piero Ventrone, kuaga dunia.

Mwitaliano huyo alikuwa sehemu ya benchi ya kiufundi ya mkufunzi Antonio Conte tangu Novemb 2021 na akawa kipenzi cha wachezaji wa Spurs.

Mechi dhidi ya Chelsea ilikuwa ya pili kwa mkufunzi Roberto de Zerbi kusimamia baada ya kuongoza Brighton kulazimishia Liverpool sare ya 3-3 katika pambano lake la kwanza tangu aaminiwe kuwa mrithi wa Graham Potter aliyesajiliwa na Chelsea baada ya Thomas Tuchel kupigwa kalamu kwa sababu ya msururu wa matokeo duni.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Gachagua asimulia jinsi Ruto alivyopata umaarufu katika...

PSG waambulia sare tasa dhidi ya Reims ligini

T L