• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Ingwe yapata mpinzani mpya Betway Cup timu ya Taita Taveta All Stars ikiachwa nje

Ingwe yapata mpinzani mpya Betway Cup timu ya Taita Taveta All Stars ikiachwa nje

Na GEOFFREY ANENE

TIKI FC imechukua nafasi ya Taita Taveta All Stars kucheza dhidi ya AFC Leopards kwenye Kombe la Rais wa Shirikisho la Soka Kenya (FKF) almaarufu Betway Cup litakaloanza kote nchini mnamo Februari 13-14.

Katika droo ya raundi ya 64-bora iliyofanywa na FKF mnamo Februari 4 jijini Nairobi, FKF ilitangaza kuwa Taita Taveta All Stars itakuwa mwenyeji wa Ingwe. Hata hivyo, ikitoa ratiba ya mechi za raundi hiyo hapo Februari 8, FKF ilikutanisha Leopards dhidi ya Tiki ambayo pia inatoka katika kaunti ya Taita Taveta na kuacha Taita Taveta All Stars nje kabisa.

Sindo United kutoka Nyanza, ambayo pia ilikuwa katika droo ya kwanza, haipo. Nafasi yake imetwaliwa na CUSCO kutoka Eldoret. Hakuna sababu imetolewa kwa mabadiliko hayo. Mashindano ya Betway Cup yanatumika kuchagua mwakilishi wa Kenya katika Kombe la Mashirikisho la Afrika (Confederation Cup).

RATIBA (64-bora):

Februari 13

KSG Ogopa na Dimba Patriots GEMS School Cambridge | Nairobi 13:00

Marafiki na JKUAT Ruringu Stadium | Nyeri 15:00

Mwatate United na Twyford Wundanyi Stadium | Taita 13:00

Tiki na AFC Leopards Wundanyi Stadium | Taita 15:15

Flamingo na Kariobangi Sharks Finlays Grounds | Naivasha 15:00

Uprising na Progressive Camp Toyoyo Grounds | Nairobi 13:00

Tandaza na MCF Camp Toyoyo Grounds | Nairobi 15:15

FC Shells na Fortune Sacco Mbaraki Grounds | Mombasa 15:00

Mutomo Tigers na Nairobi City Stars Kitui Stadium | Kitui 14:00

Transfoc na Migori Youth Kenyatta Stadium | Kitale 13:00

Elim na Ulinzi Stars Kenyatta Stadium | Kitale 15:15

Kajiado North na Nkanas GEMS School Cambridge | Nairobi 15:00

Bungoma Superstars na Zetech Titans Sudi Stadium | Bungoma 13:00

Mihuu United na Tusker Sudi Stadium | Bungoma 15:15

Vihiga Sportiff na Nation FC Mumboha Grounds | Vihiga 13:00

Luanda Villa na GDC Mumboha Grounds | Vihiga 15:15

Vegpro na SS Assad Longonot Horticulture Grounds | Naivasha 15:00

NYSA na Machakos United Nakuru Athletic Club | Nakuru 15:00

Februari 14

Sigalagala TTI na Dero Sigalagala Grounds | Kakamega 15:00

Rware na Posta Rangers Ruringu Stadium | Nyeri 15:00

Black Diamond na CUSCO Sawagongo Grounds | Yala 15:00

Alphonse na Administration Police St Sebastian Park | Muranga 13:00

Muranga Seal na Bandari St Sebastian Park | Muranga 15:15

MMUST na Bidco United Approved School | Kakamega 15:00

Nyabururu Sportiff na Keroka TTI Gusii Stadium | Kisii 13:00

Kiandege Jets na KCB Gusii Stadium | Kisii 15:15

Twomoc na Naivas Nakuru Athletic Club | Nakuru 13:00

Fussball Nax na Mara Sugar Nakuru Athletic Club | Nakuru 15:15

Kobare na Egerton Nyathi Complex | Siaya 15:00

Blessings na Equity Kenyatta Stadium | Kitale 13:00

Kitale Allstars na Sofapaka Kenyatta Stadium | Kitale 15:15

Congo Boys na Gor Mahia Mbaraki Grounds | Mombasa 15:00

  • Tags

You can share this post!

Ingwe yapata kocha wa 12 wa kigeni ndani ya miaka 12,...

Atletico Madrid wakabwa koo na Celta Vigo huku Luis Suarez...