• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Kabras walipua Monks, KCB wakinyamazisha ‘madeejay’ Homeboyz

Kabras walipua Monks, KCB wakinyamazisha ‘madeejay’ Homeboyz

Na GEOFFREY ANENE

VIONGOZI Kabras Sugar wamelipua Catholic Monks 78-0 ugani ASK Kakamega na kudumisha rekodi yao safi kwenye Ligi Kuu ya raga ya wachezaji 15 kila upande Jumamosi katika siku ambayo nambari mbili KCB pia walirarua Homeboyz 77-10 ugani KCB Ruaraka jijini Nairobi.

Wanabenki wa KCB walitoka chini 0-5 wakinyamazisha Homeboyz kupitia alama kutoka kwa Peter Waitere na Vincent Onyala (miguso miwili kila mmoja), Festus Shiasi, Michael Kimwele, Griffin Musila, Austin Sikutwa na Bob Muhatia (mguso mmoja kila mmoja) na mikwaju ya Brian Wahinya.

Homeboyz walipata alama zao kupitia miguso ya Brian Juma na Ramadhan Masete.

Katika mechi iliyotangulia kusakatwa ugani RFUEA jijini Nairobi, Nondescripts walitoka nyuma mara nne wakilima Kisumu 32-16 na kuandikisha ushindi wa kwanza msimu huu. Waliofungia ni Calvin Sheunda (penalti mbili na mikwaju mitatu) na Bruce Odhiambo, Ian Mumbwani, Oliver Tembo na Benson Saleh (mguso mmoja kila mmoja). Washington Ochieng alifungia Kisumu penalti tatu na mkwaju mmoja naye Alvin Kalori akapachika mguso mmoja.

Katika mechi ya pili ugani RFUEA, wenyeji Kenya Harlequin walitoka chini mara mbili na kubomoa Mwamba 40-10. Quins walijipata wachezaji 14 uwanjani wakati mmoja katika kipindi cha pili baada ya nyota wa Kenya Shujaa, Herman Humwa kulishwa kadi ya njano kwa kuchezea mpinzani vibaya.

Blak Blad nao walionyesha ujasiri mkubwa wa kutoka nyuma 0-19 na kugawana alama na wageni wao Nakuru katika sare ya 19-19 katika Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Menengai Oilers ilipepeta Strathmore Leos 27-10 katika mchuano mwingine mjini Nakuru.

  • Tags

You can share this post!

Maombi yakikataa kufanya kazi ‘faster’...

Gachagua alieleweka vibaya kwa kutetea Wakenya kwa miradi...

T L