• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 7:50 AM
Maombi yakikataa kufanya kazi ‘faster’ nitageukia mganga, mwanadada aamua

Maombi yakikataa kufanya kazi ‘faster’ nitageukia mganga, mwanadada aamua

NA NICHOLAS CHERUIYOT

KAMWAURA, NAKURU

MHUBIRI mmoja alidinda kuongoza maombi katika boma la mshirika wa kanisa lake, mwanadada alipomtisha kugeukia mganga maombi yake yakikosa kufanya kazi.

Kulingana na duru, mwanadada alisumbuliwa na tabia ya mumewe ya kushiriki ukware mjini anakofanya kazi na akamwalika pasta kwake na kumtaka atende miujiza au atafute huduma za mganga.

Ingawa pasta alikuwa akidai ana uwezo mkubwa wa kufanya miujiza, alisita kuomba kwani alijua huo ulikuwa mtego kwake.

“Wanaofaulu kupitia maombi yangu ni walio na imani ya juu. Tayari umeonyesha huna imani yoyote kwangu bali unatamani sana kuenda kwa mganga,” pasta aliteta kisha akaondoka baada ya kumtaka mwanadada kufanya uamuzi wa kuwa na imani na maombi au aelekee kwa mganga.

  • Tags

You can share this post!

Sina uwezo wa kupunguza bei ya mafuta – Ruto

Kabras walipua Monks, KCB wakinyamazisha ‘madeejay’...

T L