Na GEOFFREY ANENE
SHIRIKISHO la Mpira wa Vikapu Kenya (KBF) linapanga kurejelea ligi zake wikendi.
Ligi Kuu ya Wanawake, Ligi Kuu ya Wanaume pamoja na ligi za daraja ya pili zilisimamishwa kwa ghafla mnamo Machi 26. Hii ni baada ya Rais Uhuru Kenyatta kutangaza kuwa shughuli zote za michezo zisitishwe ili kuzuia maambukizi ya virusi vya corona ambayo yalikuwa yakiongezeka kwa haraka.
“Tumekuwa na mkutano wa Ligi na Mashindano. Ratiba ya mechi itatolewa Alhamisi kabla ya ligi kung’oa nanga wikendi,” alisema Katibu wa KBF, Ambrose Kisoi mnamo Jumatano.
Wanajeshi wa Ulinzi Warriors, wanabandari wa KPA, Emyba, wanabenki wa Equity na Thunder walishikilia nafasi tano za kwanza kabla ya Ligi Kuu ya Wanaume isimamishwe.