• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Kivumbi kikali kushuhudiwa robo fainali za Koth Biro

Kivumbi kikali kushuhudiwa robo fainali za Koth Biro

Na JOHN KIMWERE

KIVUMBI kikali kinatazamiwa kushuhudiwa kwenye mechi mbili za robo fainali kuwania taji la Koth Biro ugani Umeme Ziwani, Nairobi.

Mechi ya kwanza itakuwa baina ya Wenyeji Youth na Borussia FC. Nayo Mathare Combined itakutanishwa na Team Dandora. ”Hatuna hofu na wapinzani wetu bali tunajiandaa kupambana mwanzo mwisho lengo kuu likiwa kusonga mbele maana tunataka kubeba kombe,” kocha wa Team Dandora Young Oloo alisema na kutoa wito kwa wachezaji wake kumakinika kwenye mchezo huo.

Naye kocha wa Mathare Combined Elijah Omondi alikiri kuwa wanafahamu mchezo huo hautakuwa mteremko maana pande zote zimejiandaa kupambana kufa na kupona. Team Dandora chini ya nahodha, Lameck Omondi ilijikatia tiketi ya mechi hiyo ilipozaba Kingstone FC mabao 4-3 kupitia mikwaju ya penalti baada ya kutoka sare bao 1-1 kwenye mechi za 16-bora.

Mathare Combined ilipiga Huruma Kona 3-1, Wenyeji Youth ilichapa kaka zao Wenyeji United mabao 3-2 huku Borrusia FC ikizoa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Biafra Kamaliza FC. Ngarambe ya muhula huu ilishirikisha jumla ya timu 46 kutoka mitaa mbali mbali katika Kaunti ya Narobi.

Bingwa wa mwaka huu atapokea kitita cha Sh300, nambari mbili atatuzwa Sh100,000, nambari tatu na nne watatia mfukoni Sh 50,000 na Sh20,000 mtawalia.

You can share this post!

Kiini cha vyama vya Pwani kutovuma kitaifa

Ligi Kuu: KCB FC yapiga hatua baada ya kung’ata...

T L