Na MASHIRIKA
KOCHA Graham Potter, 47, alianza maisha kambini mwa Chelsea kwa sare ya 1-1 dhidi ya RB Salzburg ya Austria katika gozi la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) lililochezewa ugani Stamford Bridge mnamo Jumatano usiku.
Mkufunzi huyo wa zamani wa Brighton alitegemea pakubwa Raheem Sterling katika safu ya mbele na nyota huyo raia wa Uingereza akafunga bao katika dakika ya 48 baada ya kushirikiana vilivyo na Pierre-Emerick Aubameyang.
Mechi hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Chelsea kutandaza chini ya Potter aliyemrithi Thomas Tuchel ambaye alipigwa kalamu baada ya kikosi chake kufungua kampeni za UEFA msimu huu kwa kichapo cha 1-0 kutoka kwa Dinamo Zagreb kwenye Kundi E mnamo Septemba 6, 2022.
Chelsea kwa sasa wanavuta mkia wa Kundi E kwa alama moja baada ya AC Milan kutandika Zagreb 3-1 katika pambano jingine la Jumatano. Milan ambao ni wafalme wa soka ya Italia, watavaana na Chelsea katika mechi ijayo ya UEFA mnamo Oktoba 5, 2022 ugani Stamford Bridge.
MATOKEO YA UEFA (Jumatano):
AC Milan 3-1 Dinamo Zagreb
Shakhtar Donetsk 1-1 Celtic
Rangers 0-3 Napoli
Chelsea 1-1 RB Salzburg
Real Madrid 2-0 RB Leipzig
FC Copenhagen 0-0 Sevilla
Man-City 2-1 Borussia Dortmund
Juventus 1-2 Benfica
Maccabi Haifa 1-3 PSG
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO