• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Karua, Kalonzo wahudhuria sherehe ya Nassir kuapishwa

Karua, Kalonzo wahudhuria sherehe ya Nassir kuapishwa

NA SAMMY WAWERU

MGOMBEA mwenza wa Raila Odinga wa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya, Martha Karua na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ni kati ya wanasiasa mashuhuri wanaohudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Nassir.

Bw Nassir ameapishwa hii leo, Alhamisi katika bustani ya Mama Ngina Waterfront, Mombasa ili kuanza kutekeleza majukumu yake rasmi.

Amelishwa kiapo pamoja na naibu wake, Francis Thoya.

Gavana wa Kakamega, Fernandes Barasa na naibu wake Ayub Savula pia wameapishwa leo Jumanne katika uwanja wa Bukhungu.

Uchaguzi wa kiti cha gavana katika kaunti hizo haukufanyika mnamo Agosti 9, 2022 kufuatia dosari kwenye karatasi za kupiga kura.

Uliahirishwa mara nyingine mbili na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC); Agosti 23 na 26, hatimaye wakazi wakachaguana Agosti 29.

Bw Nassir (ODM) alimenyana na mpinzani wake, Hassan Omar aliyemezea mate ugavana Mombasa kupitia United Democratic Alliance (UDA).

Nassir aliibuka mshindi, kwa kuzoa kura 119,083 naye Omar akipata 98,108.

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka (kushoto). PICHA | KEVIN ODIT

Karua na Kalonzo, walikuwa wameandamana na mbunge Mwakilishi wa Kike wa Nairobi Bi Esther Passaris.

Mwanasiasa Martha Karua akiwa na Mbunge Mwakilishi wa Kike wa Nairobi, Bi Esther Passaris. PICHA | KEVIN ODIT

Nassir anamrithi Hassan Joho, ambaye ameongoza Mombasa mihula miwili.

Bw Joho pia amehudhuria ili kumkabidhi mrithi wake zana za uongozi.

  • Tags

You can share this post!

Matumaini ya unga wa bei nafuu yafifia

Kocha Graham Potter aanza maisha Chelsea kwa sare ya 1-1...

T L