• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Man-United walazimishia Atletico Madrid sare katika mkondo wa kwanza wa UEFA

Man-United walazimishia Atletico Madrid sare katika mkondo wa kwanza wa UEFA

Na MASHIRIKA

CHIPUKIZI Anthony Elanga, 19, aliweka hai matumaini ya waajiri wake Manchester United kutinga robo-fainali za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu.

Hii ni baada ya kinda huyo raia wa Uswidi kufunga bao la kusawazisha mwishoni mwa kipindi cha pili dhidi ya Atletico Madrid katika mkondo wa kwanza wa mchuano wa hatua ya 16-bora mnamo Jumatano usiku ugani Wanda Metropolitano, Uhispania.

“Hatua ninazoendelea kupiga katika ulingo wa soka ni miongoni mwa mambo ambayo nimekuwa nikitazamia tangu utotoni. Sitaki kumwangusha kocha wangu wala kikosi changu. Nitajitolea kwa asilimia 150 kuchezea Man-United,” akasema fowadi huyo.

Hadi Elanga aliposawazisha mambo, Atletico wanaotiwa makali na kocha Diego Simeone walionekana kuwa pazuri kushinda mechi hiyo baada ya kuwekwa kifua mbele na Joao Felix katika dakika ya saba.

Bao la Felix lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na Renan Lodi aliyemtatiza pakubwa mabeki Victor Lindelof na Harry Maguire pamoja na kipa David de Gea.

Sime Vrsaljko na Antoine Griezmann walipoteza nafasi kadhaa za kufungia Atletico bao la ushindi mwishoni mwa kipindi cha pili.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wavuvi walilia fidia ya Sh1.76b

Liverpool waponda Leeds United na kuendeleza presha kwa...

T L