• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 7:47 PM
Messi aongoza PSG kuponda Lille na kufungua mwanya wa alama 13 kileleni mwa Ligue 1

Messi aongoza PSG kuponda Lille na kufungua mwanya wa alama 13 kileleni mwa Ligue 1

Na MASHIRIKA

LIONEL Messi alifunga bao lake la pili katika Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mnamo Jumapili usiku aliposaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kukomoa mabingwa watetezi Lille 5-0 ugenini.

Ushindi huo uliwezesha PSG kufungua mwanya wa alama 13 kati yao na nambari mbili Marseille kileleni mwa jedwali la Ligue 1. PSG ambao kwa sasa wanajivunia alama 56 walijiweka kifua mbele kupitia Danilo aliyefunga mabao mawili kabla ya magoli mengine kufumwa wavuni na Presnel Kimpembe, Messi na Kylian Mbappe.

Chini ya kocha Mauricio Pochettino, PSG walishuka dimbani wakiwa na ulazima wa kujinyanyua baada ya chombo chao kuzamishwa na Nice kupitia penalti kwenye kipute cha French Cup wiki moja iliyopita.

Messi, 34, sasa amefunga mabao mawili pekee kutokana na mechi 13 za Ligue 1 tangu aagane na Barcelona mwishoni mwa msimu jana wa 2020-21. Alifunga bao lake la kwanza ligini dhidi ya Nantes mnamo Novemba na anajivunia kupachikia PSG mabao matano kutokana na mechi tano za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).

Nyota huyo raia wa Argentina anajivunia rekodi ya kufunga bao katika mechi za ushindani kila mwaka tangu 2005.

You can share this post!

Ashtakiwa kwa kuchapana juu ya chapo ya sh40

Rais ahimiza Wakenya kujiandikisha kwa bima ya afya ya...

T L