• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 10:01 PM
Ashtakiwa kwa kuchapana juu ya chapo ya sh40

Ashtakiwa kwa kuchapana juu ya chapo ya sh40

Na RICHARD MUNGUTI

MUUZAJI nyama katika Bucha iloyoko eneo la Ngara Nairobi ameshtakiwa kwa kumchapa na kumwumiza mwanamke anayeuza chapatti na chai alipokataa kulipa Sh40.

Peter Kilonzo Titus aliye na umri wa miaka 26 alikabiliwa na shtaka la kumjeruhi Bi Lorna Nyamboke. Alishtakiwa mbele ya hakimu mkuu Mahakama ya Milimani Nairobi Bi Wendy Michemi. Mshtakiwa alimsihi hakimu aamuru mlalamishi afike kortini kueleza sababu ya wao kuvurugana.

Kiongozi wa mashtaka Bw Anderson Gikunda alieleza mahakama Kilonzo alienda katika Kiosk cha Nyamboke na kuagiza kifungua kinywa cha Chai na Chapati mnamo Januari 23,2022 karibu na Hoteli ya Fig Tree.

“Mshtakiwa alikula kisha akaondoka bila kulipa,” Bw Gikunda alisema. Bi Nyamboke alienda kumdai Kilonzo Mwendo wa saa moja jioni siku hiyo lakini akachapwa. Mahakama ilifahamishwa mshtakiwa alitiwa nguvuni na kufunguliwa shtaka.

Bi Michemi alimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya pesa tasilimu Sh10,000. Mshtakiwa alimsihi hakimu ampunguzie dhamana lakini akafahamishwa kiwango alichopewa kinalingana na makosa anayodaiwa alitenda.

Kesi hiyo itatajwa baada ya wiki mbili.

You can share this post!

Kinara wa bidhaa feki aagizwa kufika kortini kuhusu barakoa...

Messi aongoza PSG kuponda Lille na kufungua mwanya wa alama...

T L