• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Mfumaji Lukas Nmecha ajiunga na Wolfsburg ya Ujerumani

Mfumaji Lukas Nmecha ajiunga na Wolfsburg ya Ujerumani

Na MASHIRIKA

FOWADI chipukizi wa Manchester City na timu ya taifa ya Ujerumani, Lukas Nmecha, amejiunga na kikosi cha VfL Wolfsburg kinachoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga).

Nmecha, 22, aliwajibikia klabu ya Anderlecht ya Ligi Kuu ya Ubelgiji kwa mkopo mnamo 2020-21 ambapo alifunga mabao 21 kutokana na mechi 41.

Mshambuliaji huyo mzaliwa wa eneo la Hamburg, aliwahi kuwakilisha Uingereza katika mapambano mbalimbali ya chipukizi kabla ya kujiunga na Man-City waliomtuma Wolfsburg kwa mkopo mnamo 2019-20.

Hadi alipoondoka Man-City, alikuwa amechezeshwa na kikosi hicho mara mbili kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na mara moja kwenye kipute cha Carabao Cup.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

KAA Gent anayochezea Okumu yachangisha Sh5.7 milioni...

Giroud awaaga Chelsea kwa shukrani tele akiungana na Tomori...