• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Mshindi wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza msimu huu kujulikana siku ya mwisho baada ya Arsenal kupepeta Spurs

Mshindi wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza msimu huu kujulikana siku ya mwisho baada ya Arsenal kupepeta Spurs

Na MASHIRIKA

MSHINDI wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) msimu huu atajulikana katika siku ya mwisho ya kampeni.

Hii ni baada ya Arsenal kupepeta Tottenham Hotspur 3-0 mnamo Jumatano usiku ugani Emirates na kusalia miongoni mwa wagombezi halisi wa taji la WSL muhula huu.

Arsenal walifunga mabao yao kupitia kwa Beth Mead na Caitlin Foord na kupunguza pengo la alama kati yao na viongozi wa jedwali Chelsea hadi pointi moja pekee. Arsenal kwa sasa wanashikilia nafasi ya pili jedwalini kwa alama 52. Manchester City wanakamata nafasi ya tatu kwa pointi 44, mbili kuliko Manchester United wanaofunga orodha ya nne-bora.

Chelsea wanalenga kuwa kikosi cha kwanza kuwahi kunyanyua taji la WSL kwa mara ya tatu mfululizo huku Arsenal wakipigania taji hilo kwa mara ya kwanza tangu 2019. Chelsea wanafukuzia pia Kombe la FA msimu huu na wamepangiwa kuvaana na Man-City katika fainali mnamo Mei 15, 2022 ugani Wembley.

Wakicheza dhidi ya Spurs, Arsenal walifungua karamu yao ya mabao kupitia kwa Mead kabla ya magoli mengine kujazwa kimiani na Jessica Naz na Maeva Clemaron.

Arsenal watakamilisha kampeni zao za msimu huu ligini dhidi ya West Ham ugani Dagenham mnamo Jumapili huku Chelsea wakialika Manchester United.

Ushindi wa Arsenal mnamo Jumatano unamaanisha kwamba Spurs sasa hawajashinda mechi saba mfululizo katika WSL. Hata hivyo, wanashikilia nafasi ya tano kwa alama 29, mbili zaidi kuliko West Ham United. Spurs watakuwa wenyeji wa Leicester City katika mechi ya mwisho msimu huu.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Pasta ashtakiwa kwa ulaghai wa mafuta ya utakaso

Uhalifu: Mishi alaumu wanaume kuzembea

T L