CHARLES ONGADI
RATIBA ya awamu ya tatu ya mashindano ya ndondi ya Africa Zone 3 yanayoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetolewa.
Christine Ongare anatarajiwa kurudi ulingoni dhidi ya Munga Zalia wa DRC huku Stacy Ayoma akikabiliana na Yumba Therese pia wa DRC.
Elizabeth Akinyi atachubuana sura na Makwikila Hellene wa DRC naye Elizabeth Andiego akimkabili Rudy Gramane wa wa Msumbiji.
David Karanja atakutana na Nimuboma Moussa wa Burundi katika uzani wa fly. Shaffi Bakari naye atakabiliana na Oka Shash wa Liberia katika pigano lingine la fly.
Joseph Shigali atakabiliana na Shengue Allain wakati Boniface Mogunde akipepetana na Mpiana Kalumbu katika welter.
Katika Middle Edwin Okongo atacharazana na Mougndza Styven huku George Cosby Ouma akikutana na El Magasbi wa Libya.
Hezron Magangha atachuana na Nkulu Pogba wa DRC katika lightheavy naye Joshua Wasike akikung’utana na Mutombo Jeonash wa DRC huku Elly Ajowi akirudi jukwaani kukwaruzana na Saad Saad wa Liberia.