• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 4:25 PM
Oliver Solberg halali akiota kufuata nyayo za babaye Petter Solberg kwenye Safari Rally

Oliver Solberg halali akiota kufuata nyayo za babaye Petter Solberg kwenye Safari Rally

Na GEOFFREY ANENE

DEREVA nyota Oliver Solberg ana ari kubwa ya kufuata nyayo za babaye akinuia kushiriki mbio za Safari Rally zitakazorejea kwenye Mbio za Magari za Dunia (WRC) mwezi Juni baada ya miaka 19.

Katika mahojiano na tovuti ya michezo ya Kawowo nchini Uganda, Solberg alikiri kuwa familia yake haijakamilisha biashara yake kwenye mbio hizo ngumu za magari zitakazofanyika katika kaunti za Nairobi na Nakuru.

Solberg ana imani tele ya kushindana katika mbio za Safari Rally, ambayo ni mojawapo ya ndoto zake.

Mtoto huyu wa bingwa wa dunia wa mwaka 2003 Petter Solberg anakumbuka kazi babaye na anatumai kuandikisha historia yake mwenyewe.

Petter alishinda Safari Rally mwaka 1999 akishiriki duru hiyo ya Kenya kwa mara ya kwanza kabisa akiendesha gari la Ford Focus.

“Safari Rally ni mojawapo ya mbio za magari natamani kushiriki. Babangu ana hadithi nyingi kutoka kwa duru hiyo.

“Nimeona video kadhaa za wanyama na sehemu zenye mandhari ya kuvutia. Itakuwa kitu cha kujivunia nikijionea mwenyewe mashindanoni,” alisema Oliver.

Dereva huyu mwenye umri wa miaka 19 amekuwa na safari nzuri katika ukuaji wake wa dereva nyota. Tayari anamezewa mate na timu ya magari ya Hyundai.

  • Tags

You can share this post!

Harambee Stars yalenga Misri baada ya mechi ya kirafiki...

Tundu Lissu asema atarejea Tanzania iwapo ataruhusiwa...