• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 1:20 PM
Olunga afunga mabao mawili Al Duhail ikitinga nusu-fainali Ooredoo Cup

Olunga afunga mabao mawili Al Duhail ikitinga nusu-fainali Ooredoo Cup

NA GEOFFREY ANENE

Mshambulizi matata Michael Olunga alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia Al Duhail kuzamisha Al Rayyan 3-0 na kuingia nusu-fainali ya Kombe la Qatar Stars (Ooredoo Cup) uganiĀ Al Egla 4 nchini Qatar, Jumamosi usiku.

Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Kenya alifungua ukurasa wa magoli dakika ya tano. Al Duhail almaarufu Red Knights walikuwa 2-0 juu wakati wa mapumziko baada ya Olunga kuongeza la pili dakika ya 36.

Olunga sasa ana mabao 14 katika michuano 11 kwenye mashindano yote msimu huu. Suhab Gannan alifuma wavuni bao la tatu dakika ya 51.

Katika mechi zingine zilizosakatwa Jumamosi, Al Sadd waliuma Al Ahli Doha 4-0 kupitia mabao ya Baghdad Bounedjah (matatu) na Rodrigo Tabata uwanjani Jassim Bin Hamad mjini Doha.

Al Wakrah walilemewa 5-3 mikononi mwa Umm Salal ugani Al Janoub mjini Al Wakrah.

Mabingwa watetezi Al Sailiya waliendelea kusikitisha baada ya kupoteza 2-0 dhidi ya Qatar SC uwanjani Hamad bin Khalifa mjini Doha.

Al Markhiya walizamisha Shamal 3-2 uwanjani Al Ersal 2 huku Al Arabi wakapiga Al Gharafa 1-0 katika Chuo Kikuu cha Qatar. Timu zingine zilizotinga nusu-fainali ni Umm Salal na Al Arabi.

Umm Salal wanaongoza Kundi A kwa pointi 12 baada ya mechi nne za kwanza wakifuatiwa na Al Sadd (pointi tisa), Qatar SC (sita), Al Ahli (sita), Al Wakrah (tatu) na Al Sailiya (sifuri).

Al Duhail wamekaa juu ya Kundi B kwa pointi 10 na kufuatiwa na Al Arabi (tisa), Al Gharafa (tano), Al Rayyan (nne), Al Shamal (nne) na Markhiya (moja).

Umm Salal na Al Duhail ndio timu pekee hazijapoteza mechi kwenye kipute hicho ambacho mechi zijazo ni Oktoba 14-15.

  • Tags

You can share this post!

Ruto ayataka mataifa ya EAC kuondoa vikwazo vya kibiashara...

Borussia Dortmund watoka nyuma na kulazimishia Bayern...

T L