• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 12:11 PM
Borussia Dortmund watoka nyuma na kulazimishia Bayern Munich sare ya 2-2 katika Bundesliga

Borussia Dortmund watoka nyuma na kulazimishia Bayern Munich sare ya 2-2 katika Bundesliga

Na MASHIRIKA

BORUSSIA Dortmund walitoka nyuma kwa mabao 2-0 na kulazimishia Bayern Munich sare ya 2-2 katika gozi kali la Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) lililowakutanisha ugani Signal Iduna Park mnamo Jumamosi.

Anthony Modeste alisawazishia Dortmund katika dakika ya 94, sekunde chache baada ya Kingsley Coman wa Bayern kuonyeshwa kadi nyekundu. Awali, Youssoufa Moukoko alikuwa amerejesha Dortmund mchezoni kwa kuwafungia bao la kwanza katika dakika ya 74.

Bayern walifungua ukurasa wa mabao kupitia Leon Goretzka na Leroy Sane walioandalia krosi safi na chipukizi Jamal Musiala.

Coman alionyeshwa kadi ya manjano kwa kosa la kumchezea Jude Bellingham visivyo na akaonyeshwa nyekundu mwishoni mwa kipindi cha pili baada ya kumkabili Karim Adeyemi vibaya.

Dortmund walimwaminia chipukizi Bellingham utepe wa unahodha katika pambano hilo baada ya Matt Hummels kuondolewa uwanjani katika kipindi cha pili. Matokeo hayo yalisaza Dortmund katika nafasi ya nne jedwalini kwa alama 16 sawa na Bayern ambao pia wamesakata mechi tisa.

Ni pengo la pointi moja ndilo linatamalaki kati ya miamba hao na SC Freiburg na Union Berlin wanaoongoza jedwali baada ya kutandaza michuano minane kila mmoja.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Olunga afunga mabao mawili Al Duhail ikitinga nusu-fainali...

Askofu apongeza serikali kwa kufunga baa za kero tele...

T L